Posts

2. Hosiana, Mesiya

  Hosiana, Mesiya Aingia mjini kwake Fagieni popote, Zipambeni njia zote; Tandikeni mauwa, Aingie na shwangwe. Hosiana,Mwokozi Njoo, twakungojea Bwana. Tumepamba nioyo, Twakukaribisha kwetu. Tunakufungulia, milango ya mioyo Hosina, ee shujaa! Utusaidie sisi, Tuwe wako kwa kweli Tukutumikie vema. Kwani hutakubali Watu wasio kutii. Hosiana, Mfalme mkuu! Uingie kwetu hima! Uliebarikiwa, Uingie mlango wetu. Hosiana, karibu! Bwana, njoo! Haleluya!

3. Sayuni, ufuhi!

Sayuni, ufurahi! Shangilia yerusalemu! Yuaja mfalme wako, Mwenye amani kwako. Sayuni hufurahi! Shangilia yerusalemu. Hosiana, Mesiya Utubariki sasa. Jenga ufalme wako Ulimwenguni mwote. Hosiana, Mesiya Utubariki sasa. Hosiana! Pongezi! Twakuamkia bwana! Kiti cha enzu yako Chasimama milele. Hosiana! Pongezi! Twakuamkia Bwana!

4. Fungua Milango Yote

Fungua milango yote Yuaja Bwana wa mbingu, Mfalme wa wafalme wote, Mwokozi wa ulimwengu. Atuletea uzima; Kwahiyo tumuimbieni; Tumsifuni Mungu, Aliye tuumba. Ni mwenye haki na shujaa Uple mwingi amevaa; Rehema ni taji yake; Huruma ni fimbo yake; Atuondolea shida. Kwahiyo tumuimbieni; Tumsifuni Mungu, Mwokozi watu mkuu. Miji na nchi Huchipuzwa, Afikako Mfamle huyu; Nayo mioyo huchekeshwa, Anayo ingia Yesu. Ndio jua la furaha Linalo tufurahisha. Tumsifuni Mungu Mtunza mioyo yetu. Fungua milango yote! Tengenezeni mioyo! Makuti yawe upole, Furaha, pendo, amni. Mwokozi ata wajia, Aleta raha, uzima. Tumsifuni Mungu, Ni mwenye rehema. Njoo, mwokozi wangu Yesu, Nakufungulia moyo. Uingie na rehema, Nione upole wako. Uniongoze kwa roho, Nifike kwako Mbinguni. Jina lako Bwana Lisifiwe pote.

5. Nikulakije Vema

Nikulakje vema Bwan wangu Yesu Wote wanakungoja Wapewe uzima. Nuru yako ing’aze Hata moyo wangu. Nijue mabo mema, Yakupendezayo. Wamekutandikia Mauwa na nguo. Name nakuimbia Nyimbo za furaha. Moyo ukupendeze Kwa sifa na nyimbo, Ukakutumikie Sikuzangu zote Umetoka Mbinguni Ukawa masikini Ukaacha fura Utupe uzima. Natulipo nyang’anywa Ufalme na raha, Ukaja mponya wetu Kuturudishia. Nalifungwa na mwovu, Ukanifungua. Nikawa nimetwezwa, Ukanitukuza, Ukanifanya mkubwa, Ukanipa mali, Zisizo malizika, Kwa kutu na wezi. Umenijia mimi, Sababu ya nini? Sababu ya kupenda Uwaponye wote Waonao huzuni Kwa makoso yao Wakijuta kwa kweli, Utawapokea. Ushike neon hili, Umati wa Yesu, Ukiwa na huzuni Na shida popote. Usiogope kitu; Wokovu tayari. Anaye tufariji Yukaribu sasa.

6. Wakristo, Iwekeni

Wakristo, iwekeni Mioyo tayari. Yesu awaingie, Ni Mwokozi wenu. Mungu amemtuma Kwa neema na rehema Atuletee sisi Uzima na nuru. Mwokozi ana kuja, Mlimieni njia! Mioyo iwe safi Acheni matendo Yanayomchukiza. Lijazwe kila bonde, Milia ipunguzwe Mioyoni mwenu. Ukiwa mnyenyekevu, Wapendwa na Mungu. Ukiwa na kiburi, Utaangamizwa. Ukimtumikia, Mungu kwa mwendo mwema Umpendezao yeye, Yesu akupenda. Uniweke tayari Niliye maskini, Ee Yesu siku hizi Kwa rehema yako Ingia moyoni, Ukinijia sasa. Nami nitakusifu Kwa kinywa na moyo.

7. Moyo Wangu Sikiliza

Moyo wangu sikiliza Habari njema hii Ya wokovu mkubwa. Sikia kuimbwa kwao Malaika na watu: “yesu azaliwa.” Mponya amekuja leo Kutoka mbinguni, Aokoe watu. Mungu wetu ameshuka, Akawa mwana mtu Kwa ajili yetu. Na sasa yumo zizini, Aita: “njooni Hima kwangu wote, Nawaondolea ninyi Uchungu wowote, Muwe na furaha.” Basi tumwendee hima Wakumbwa wadogo, Njooni wote sasa! Awe mwanga wetu. Wenyeshida na ukiwa njooni, Awape neema yake Mungu, Yeye ana mali nyingi, Dhahabu na fedha Za mioyo yenu. Ninakaa ulimwenguni Lakini napenda Kuhamia kwako. Mwisho niwe furahani Pamoja na wewe mwenye utukufu.