4. Fungua Milango Yote
Fungua milango yote
Yuaja Bwana wa mbingu,
Mfalme wa wafalme wote,
Mwokozi wa ulimwengu.
Atuletea uzima;
Kwahiyo tumuimbieni;
Tumsifuni Mungu,
Aliye tuumba.
Ni mwenye haki na shujaa
Uple mwingi amevaa;
Rehema ni taji yake;
Huruma ni fimbo yake;
Atuondolea shida.
Kwahiyo tumuimbieni;
Tumsifuni Mungu,
Mwokozi watu mkuu.
Miji na nchi
Huchipuzwa,
Afikako Mfamle huyu;
Nayo mioyo huchekeshwa,
Anayo ingia Yesu.
Ndio jua la furaha
Linalo tufurahisha.
Tumsifuni Mungu
Mtunza mioyo yetu.
Fungua milango yote!
Tengenezeni mioyo!
Makuti yawe upole,
Furaha, pendo, amni.
Mwokozi ata wajia,
Aleta raha, uzima.
Tumsifuni Mungu,
Ni mwenye rehema.
Njoo, mwokozi wangu Yesu,
Nakufungulia moyo.
Uingie na rehema,
Nione upole wako.
Uniongoze kwa roho,
Nifike kwako Mbinguni.
Jina lako Bwana
Lisifiwe pote.
Comments
Post a Comment