6. Wakristo, Iwekeni
Wakristo, iwekeni
Mioyo tayari.
Yesu awaingie,
Ni Mwokozi wenu.
Mungu amemtuma
Kwa neema na rehema
Atuletee sisi
Uzima na nuru.
Mwokozi ana kuja,
Mlimieni njia!
Mioyo iwe safi
Acheni matendo
Yanayomchukiza.
Lijazwe kila bonde,
Milia ipunguzwe
Mioyoni mwenu.
Ukiwa mnyenyekevu,
Wapendwa na Mungu.
Ukiwa na kiburi,
Utaangamizwa.
Ukimtumikia,
Mungu kwa mwendo mwema
Umpendezao yeye,
Yesu akupenda.
Uniweke tayari
Niliye maskini,
Ee Yesu siku hizi
Kwa rehema yako
Ingia moyoni,
Ukinijia sasa.
Nami nitakusifu
Kwa kinywa na moyo.
Comments
Post a Comment