5. Nikulakije Vema
Nikulakje vema
Bwan wangu Yesu
Wote wanakungoja
Wapewe uzima.
Nuru yako ing’aze
Hata moyo wangu.
Nijue mabo mema,
Yakupendezayo.
Wamekutandikia
Mauwa na nguo.
Name nakuimbia
Nyimbo za furaha.
Moyo ukupendeze
Kwa sifa na nyimbo,
Ukakutumikie
Sikuzangu zote
Umetoka Mbinguni
Ukawa masikini
Ukaacha fura
Utupe uzima.
Natulipo nyang’anywa
Ufalme na raha,
Ukaja mponya wetu
Kuturudishia.
Nalifungwa na mwovu,
Ukanifungua.
Nikawa nimetwezwa,
Ukanitukuza,
Ukanifanya mkubwa,
Ukanipa mali,
Zisizo malizika,
Kwa kutu na wezi.
Umenijia mimi,
Sababu ya nini?
Sababu ya kupenda
Uwaponye wote
Waonao huzuni
Kwa makoso yao
Wakijuta kwa kweli,
Utawapokea.
Ushike neon hili,
Umati wa Yesu,
Ukiwa na huzuni
Na shida popote.
Usiogope kitu;
Wokovu tayari.
Anaye tufariji
Yukaribu sasa.
Comments
Post a Comment