95. Bwana Yesu Alikufa



Bwana Yesu alikufa kwa sababu

yetu sisi, alipata duniani

maumivu mengi sana.


Bustanini akiomba akafadhaika

kabisa. Jasho lake kama damu

nchini ikadondoka.


Wayuda wakamwendea, wakamshika,

wakamfunga, na rafiki zake wote

wakimbia, wakamwacha.


Na wale wakampeleka barazani

kumhukumu. Wamhukumu yule mfalme,

atakayewahukumu.


Wakamfyonza, wakampiga,

wakampeleka Golgota,

pale wakamwamba mtini,

kwa misumari kumkaza.


Kukawa na giza huko,

nchi ikatetemeka.

Watu walioko wote,

wakaona woga mwingi.


Na saa tisa ikifika,

Yesu apaza sauti kuu, kwamba:

Yamemalizika; mara akakata roho.


Askari wakamwendea,

wakamwona amekufa.

Nao wakamchoma mkuki;

ukapenya moyo wake.


Damu yake ikatoka,

yakatoka maji tena.

Maji, damu iwezayo

kuosha uchafu wote.


Na watu wema wamshusha,

wamfunga katika sanda,

wakamweka kaburini,

na penye mlango jiwe kuu.


Siku ya tatu atoka

Yesu Kristo kuzimuni,

alivyotangaza kwanza,

yu mzima hata milele!

Comments

Popular posts from this blog

72. Tumesikia Mbiu

51. Yesu Ndiye Kiongozi Wangu