51. Yesu Ndiye Kiongozi Wangu
Yesu ndiye kiongozi
Wangu,
Kumfuata yeye ni furaha,
Ajuaye kuongoza vema,
Anilinda, nisione shida,
Analeta raha moyoni.
Bwana yesu
Akiniogoza,
Nitapita pori na misitu,
Nitavuka mito na bahari
Kwa furaha,
Kwani nina njia
Yakufika mjini kwa Mungu.
Nikilala Yesu anilinda,
Anitunza yeye siku zote.
Hata nikifika njia panda,
Nikiona shaka, aonyesha
Njia ya kufika kwake.
Siku zote namfuata yeye,
Sitaona kiu wala njaa;
Anitunza kwa rehema
Nyingi;
Nitaweka mikononi mwake
Moyo wangu, auokoe.
Comments
Post a Comment