94. Unipe Nguvu Bwana
Unipe nguvu, Bwana nikumbuke
mateso yako yaliyokupata,
kutukomboa tulioanguka katika dhambi.
Umemtii Baba, mpaka kufa kwako
mahali petu ulisulubishwa,
makosa yetu yalikuwa mengi, umetufia.
Wokovu wangu ulinitafuta;
nakuangukia Mwokozi wangu,
nakushukuru nikiitazama huruma yako.
Comments
Post a Comment