190. Onjeni, Onjeni



1. K: Onjeni, onjeni. 

W: Onjeni muone kuwa Bwana ni mwema, onjeni. 

K:heri. W:Anayemtumaini, 

K: Heri 

W:Anayemtumaini, ni heri.


2. K: Mcheni, mcheni. 

W: Mcheni Bwana, mlio watakatifu, mcheni.

 K:Wale 

W: Wanaomcha Bwana 

K:Wale 

W:Wanaomcha Bwana ni heri.


3. K: Na samba, na samba. 

W: Na samba hutindikiwa, huona njaa na samba. 

K: Bali 

W: Wamtafutao Bwana, 

K: Hawa 

W: Hawahitaji kitu, chochote


4. K: Njooni, njooni, 

W: Njooni, enyi wanangu, nisikilize njooni. 

K: Nanyi 

W: Mtamjua Bwana, 

K: Nanyi 

W: Mtamjua Bwana, njooni


5. K: Ni nani, ni nani? 

W: Ni nani apendezwaye nao uzima, ni nani? 

K: Mwenye 

W: Kupenda siku nyingi,

 K: Mwenye 

W: Kupenda siku nyingi za mema.


6. K: zuia, zuia. 

W: Zuia ulimi, sema yaliyo kweli, zuia. 

K: Hata 

W: Htaa midomo bila hila 

K: Hata 

W: Midomo bila hila, zuia.


7. K: Uache

 W: Uache mabaya tenda mapenzi yake, uache

 K: Nawe 

W: Ufate amani, 

K: Nawe 

W: Utafute amani, amani.

Comments

Popular posts from this blog

72. Tumesikia Mbiu

51. Yesu Ndiye Kiongozi Wangu