9. Faraja, Tumaini Langu
Faraja tumaini langu
Usiniache gizani,
Moyo ni wazi kukungoja,
Ee Yesu uniingie,
Furaha ya mbingu na nchi,
Mwana Adamu na Mungu;
Ee nuru kutoka mbinguni,
Angaza moyo wangu huu.
Mototo mpendwa,
Nakuomba,
Chagua moyo wangu huu,
Ufanye kuwa horilako
Ukalazwe humo wewe.
Ili nipate mwisho mwema
Wa shida yangu na vita.
Zaliwa ndani yangu Yesu,
Na ndani yangu ukuwe.
Mwokozi wangu utulize
Tumaini hili kubwa.
Ukija nitakupokea
Kwa roho nyenyekevu, hii.
Uweza wangu wote pia
Wakungojea kwa uchu.
Nataka kukutumikia:
Njoo, Yesu usikawie .
Comments
Post a Comment