88. Nataka Kusimama



Nataka kusimama

Chini ya msalaba,

Kama kivuli cha mwamba

Wakati wa mchana,

Kama ni maji nyikani,

Kambi safarini,

Na hapa nitapumzika,

Kwani jua kali.


Mahali pema sana

Chini ya msalaba,

Kwani hapo waoneka

Upendo wa Yesu.

Yakobo alivyoona

Ndotoni zamani,

Mti Yesu aliowambwa,

Ni ngazi kwa Mungu.


Juu ya msalaba huo

Yesu alikufa.

Alikufa tuokoke,

Tuliopotea.

Ninastaajabu kabisa

Ni mambo mawili:

Kwake Yesu ni upendo,

Kwangu mimi kosa!


Wataka kuonana

Na Yesu Mbinguni,

Yakupasa kukaa kwanza

Chini ya mti huo.

Ni kwake siku chache tu

Mateso na shaka.

Halafu pasipo mwisho

Furaha kwa Bwana!

Comments

Popular posts from this blog

72. Tumesikia Mbiu

51. Yesu Ndiye Kiongozi Wangu