84. Nimshangilie Bwana Wangu



Nimshangilie Bwana wangu

Na kumwimbia Mkombozi

Katukomboa msalabani,

Nisifu pendo lake kuu

Haya mwimbieni Yesu,

Amekubali mateso,

Katukomboa msalaabani,

Tusifu pendo lake kuu!


Tumsifu yeye

Mponya wetu

Katika ulimwemgu huu,

Katupatanisha na baba,

Tulio wakosaji tu.

Haya mwimbieni …


Katuletea mwanga wake,

Tulikaa katika giza,

Wokovu ukaonekana,

Kamshinda mwovu,

Ni shujaa!

Haya mwimbieni …


Na tumtukuze Bwana wetu,

Tumtumikie kwa bidii,

Na atawale apendavyo,

Na sisi sote tutamtii!

Haya mwimbieni …

Comments

Popular posts from this blog

72. Tumesikia Mbiu

51. Yesu Ndiye Kiongozi Wangu