81. Ulimwengu Tazama



Ulimwengu tazama,

Yesu Mwokozi wako asulubiwavyo,

Mwenye heshima yote anayavumilia

Mateso tena matusi.


Karibia tazama maungo yake

Yote yatokavyo damu.

Na moyo wake mwema

Kwa shida na uchungu

Unaungua vigumu.


Nani akupigaye,

Aliyekufanyia

Mambo kama haya?

Wewe huna makosa

Kama wengine wote,

Hujui kosa lolote.


Makosa yangu mimi

Yaliyo kama mchanga

Hayahesabiki,

Ndiyo yakutiayo mateso

Na uchungu

Uliyo ya vumilia


Mimi nimestahili

Kulipa haya yote,

Na kufungwa sana.

Mapigo na mateso

Uliyopata wewe

Yalitoka kwangu mimi.


Umenitwika mzigo

Ulio mzito sana

Kuliko jiwe kuu.

Wachukua maovu,

Tupate kuokoka

Tukae nawe daima!

Comments

Popular posts from this blog

72. Tumesikia Mbiu

51. Yesu Ndiye Kiongozi Wangu