80. Liko Neno Moja Nipendalo



Liko Neno moja nilipendalo

Ni chakula cha moyo;

Neno hili linanituliza

Nikipatwa na shida:

Kumtazama Bwana wetu pale,

Atoapo jasho kama damu,

Akubalipo mzigo,

Baba aliomtwika.


Siku zote namkumbuka yeye,

Alivyosulubishwa,

Akivumilia taabu kimya

Kama mwana wa kondoo.

Name akanikumbuka mimi,

Alisema: yamemalizika!

Huko aliniteka,

Name niwe mtu wake.


Bwana wangu u mwenye huruma,

Mimi ni mkosaji tu;

Nilipokuwapo oenye giza

Wewe ukatokea,

Ukamtafuta kondoo wako,

Kabla mimi sijakusikia.

Watoa ukombozi

Unipao uhuru.


Ndimi huru lako,

Bwana Yesu,

Wewe ndiwe Bwanangu.

Jina lako, boea liung’aze

Moyo wangu vizuri.

Amani yako nikae nayo,

Siku zangu zote mpaka kufa.

Ndivyo ninavyoomba,

Bwana unikubali.

Comments

Popular posts from this blog

72. Tumesikia Mbiu

51. Yesu Ndiye Kiongozi Wangu