78. Mwokozi Wangu Umekosa Nini?
Mwokozi wangu umekosa nini?
Wahukumiwa kama mwuaji.
Umeshtakiwa makosa
Mangapi uliyotenda?
Wapigwa sana,
Miiba taji lako,
Umetemewa mae,
Watukanwa,
Wanyweshwa nyongo
Tena siki kali,
Sababu gani
Unateswa hivi?
Makosa yangu yanakuumiza;
Mateso haya yako yanipasa,
Mimi mkosaji.
Ajabu kwabwa
Sana tendo lako;
Mchungaji unateswa kwa ajili ya kondoo,
Bwana
Unawalipia watumwa wako.
Tulipokuwa mateka
Wa mwovu,
Nawe ukaja ukatukomboa.
Tulistahili kufa kwa milele,
Ukatufia.
Mwokozi wangu nifanyeje mimi,
Niitangaze pote sifa yako?
Nakufuata nikutumikie
Maisha yote.
Comments
Post a Comment