76. Mwana Kondoo Ayalipa



Mwana Kondoo ayalipa

Madeni ya dunia.

Ayachukua makosa

Ya wakosaji wote.

Aenda na kuugua,

Anakubali kuchinjwa,

Furaha aziacha.

Wanamhukumu wampiga,

Wanamtukana wamtesa,

Asema: nakubali.


Mwana Kondoo ni Mwokozi

Ni Mponya wa mioyo;

Aliyetumwa na Mungu

Awakomboe watu.

Mwanangu, nenda okoa

Watoto niliotupa.

Sababu ya makosa.

Dhambi zao ni nyingi mno;

Watolee ukombozi

Damu na mwili wako.


“Tayari mimi, Babangu,

Nitwishe nichukue,

Maneno uyasemayo

Nitafuata yote”

Pendo hili kubwa sana,

Lamsjika Baba wa mbingu

Amtoe mwana wake.

Pendo hili lina nguvu,

Linamlaza kaburini

Aletaye uzima.


Sitasahau pendo hili

Bwanangu siku zote,

Nitakushika daima,

Kama unishikavyo.

Mwanga war oho ni wewe;

Roho inapozimia

Niwie moyo wangu.

Na tuagane, Bwanangu,

Na halafu mbingini.

Comments

Popular posts from this blog

72. Tumesikia Mbiu

51. Yesu Ndiye Kiongozi Wangu