65. Yesu ni Mponya



Yesu ni Mponya,

Aleta furaha!

Mwanzo na mwisho

Wa vyote ndiye.

Mwana Adamu

Na Mungu wa kweli

Ametujia atubariki.

Mbingu, dunia,

Toeni habari:

Yesu ni Mponya,

Aleta furaha!


Yesu ni Mponya

Aleta wokovu!

Sikilizeni habari njema!

Sisi tulipomwacha

Mungu wetu

Akaturudisha tena kwake.

Ametufanya watoto

Wa Mungu. Yesu ni Mponya

Aleta wokovu.


Yesu ni Mponya,

Aleta uzima

Kamba za kufa zimekatika.

Mwana wa Mungu

Kumshinda Shetani,

Awakomboe watumwa wake,

Amewapata, kawapa uhuru.

Yesu ni Mponya,

Aleta uzima


Yesu ni Mponya,

Mchungaji wa kweli,

Amaye lisha vizuri kondoo.

Wote walio mbali awaita,

Awarudishe kundini mwake.

Awakomboa kondoo kuani:

Yesu ni Mponya

Mchungaji wa kweli.


Yesu ni Mponya

Na mfalme wa enzi!

Mbingu zimsifu na watu wamtii

Anageuza mioyo ya watu,

Hata na sisi tumpe yetu,

Kwani apenda kutupa uzima.

Yesu ni Mponya

Na Mfalme wa enzi!


Yesu ni Mponya

Na mwenye upendo!

Anatupenda

Kwa moyo wote.

Yeye mwenyewe.

Upendo wa kweli,

Aliyekufa kwa kutupenda.

Nasi tumpendaye kwa nguvu ya roho!

Yesu ni mponya na mwenye upendo.

Comments

Popular posts from this blog

72. Tumesikia Mbiu

51. Yesu Ndiye Kiongozi Wangu