62. Uamke Kwetu Tena Roho
Uamke kwetu tena Roho
Wa mashahidi wale kwanza,
Waliolesha siku zote,
Waliomshinda Yule adui,
Wakihubiri Neno la Yesu
Kwa watu wa ulimwengu wote.
Uwashe moto wa Upendo,
Uendelee pote kuwaka.
Peleka watu mavunnoni,
Wanao fanya kazi kwa bidii.
Bwana mwenye mavuno,
Tazama:
Watenda kazi yako ni haba.
Mwanao ametuagiza
Kuomba hivi kwa Jina lake,
Na sisi wanafunzi wake,
Twashika Neno Lake kwa bidii.
Twaomba hivi kwa moyo wote.
Ee Bwana usikie, ufanye!
Utume watu wengi sana,
Walitangaze Neno kwa nguvu.
Tusaidie, tuokoe;
Ufalme wa Shetani uishe.
Usimamishe, Bwana wa mbinguni,
Ufalme wako
Ulimwenguni!
Utume mwema na uende
Mahali popote huku nchini.
Wadiini zote waingie,
Kundini mwako mwa wateule.
Amsha nao Wana wa ahadi
Na wa Imani zote wakutii.
Comments
Post a Comment