61. Sifuni Nyote Huruma



Sifuni nyote huruma ya Mungu,

Kwa nyimbo nzuri,

Umati wa Yesu!

Atualika furahini:

/:Msifuni Bwana kwa neema yake:/


Yeye ni Mfalme

Anaye tawala;

Viumbe vyote

Vinamtumikia,

Hata malaika,

Wamwabudu,

/:wanambwimbia kwa sauti nzuri:/


Enyi amataifa,

Hofu iacheni!

Njooni kwa Yesu,

Mchunga kondoo mwema.

Sikilizeni Neno lake:

/:Atukomboa kwa kufa kwake:/


Awapa watu chakula chochote,

Atushibisha kama baba mzuri,

Aleta jua hata mvua,

/:Atubariki kwa wema wake:/


Sifuni nyote huruma ya Mungu,

Kwa nyimbo nzuri,

Umati wa Yesu!

Sasa  huzuni twaishinda:

/:Msifuni Bwana neema yake!:/

Comments

Popular posts from this blog

72. Tumesikia Mbiu

51. Yesu Ndiye Kiongozi Wangu