60. Ufalme wa Mungu



Ufalme wa Mungu

uenee popote!

Nguvu yako iokoe

wakaao gizani.

Uondoe woga wote,

ukawape watu uzima,

ufalme wa Mungu.

Ushinde upesi!

Uharibu ufalme

wa shetani duniani,

ndiye mfalme wa giza.

Nawe utamshinda yeye,

Kwani una nguvu ya Mungu

Ushinde upesi!


U Shujaa wa Mungu!

Kwa rehema ya Bwana

urudishe watu wako’

wapendane kwa moyo,

wawe raia wako pote.

Ndipo utatukuzwa sana!

U shujaa wa Mungu!


Duniani popote

jina lako livume

nguvu zako zi sifiwe

na makabila yote,

uliowatengemaza,

mpaka utakapo tawala

duniani popote!


Shikeni amri hii:

Tangazeni popote

kwa makabila yoyote

neno lenye furaha,

wapate kuokolewa.

Yesu alivyotuagiza.

Shikeni amri hii!


Sifuni rehema

Ya kuokoa watu!

Tukimtumikia Bwana.

azibariki kazi

zote za mikono yetu;

Amani kuu iwe kwetu.

Sifuni rehema!

Comments

Popular posts from this blog

72. Tumesikia Mbiu

51. Yesu Ndiye Kiongozi Wangu