58. Jina Moja ni Kubwa sana
Jina moja ni kubwa sasa;
Ni jina lako Bwanangu!
Nasifu jina hili lako,
Yesu Kristo u Mwokozi.
Li tamu kwangu jina hili,
Jina lingine silijui.
Naliandika jina hili
Rohoni mwangu kabisa.
Silisahau siku zote,
Halifutiki moyoni.
Li tamu kwangu jina hili,
Jina lingene sitafuti.
Jina hili ni jua langu
Lawaka ndani ya roho.
Lanipa na utengemano,
Lafuta makosa yote.
Li tamu kwangu jina hili,
Jina linguine sifahamu.
Jina hili ni boma langu,
Upanga wangu vitani,
Ni ngao yangu na silaha,
Lamshinda hata Shetani.
Li tamu kwangu jina hili,
Jina linguine silitaki.
Jina hili lanipa nguvu,
Niweza kwenda kwa haki.
Ujuzi wote umo humo
Katika jina la Yesu.
Li tamu kwangu jina hili,
Jina linguine sitamani.
Ee Yesu, jina lako ndilo
Furaha yangu nikifa.
Ni cheti cha kuingilia
Mbinguni kwa Bwana
Mungu
Ndipo nitalisifu sana,
Jina linguine silijui.
Comments
Post a Comment