56. Mmoja ni Mfalme



Mmoja ni mfalme shujaa,

Ni mshindaji!

Enyi adui, kimbieni tu!

Nawe Sayuni uone furaha

Ukapumzishe kabisa moyo:

Uzima, utengemano, furaha

Ndizo Mwokozi

Atakazokupa.


Twende kuonja maji ya uzima

Tunayopewa na Bwana Yesu,

Aliyesema

‘’Njooni kwangu wote,

Nitapumzisha mioyo yenu’’

Nyweni, wapenzi, katika

Kisima

Chenye wokovu wa wenye

Huzuni.


Mfalme wa mbigu

Ataka kuwapa

Kilemba kizuri cha urembo,

Awawekea viti vya milele,

Heshima hiyo ni ya kushinda.

Vumilieni tabu na shida:

Yesu mwenyewe ni tuzo la

Vita.


Nguvu, ujuzi, heshima

Na sifa

Ni zake Mungu na Mwamwa

Wake.

Name nataka kufika

Mbinguni!

Nifunguliwe  mafungo yangu!

Mwenye upendo atanisikia.

Wenye uzima wanamsifu

Mungu.

Comments

Popular posts from this blog

72. Tumesikia Mbiu

51. Yesu Ndiye Kiongozi Wangu