55. Mmoja Ndiye



Mmoja ndiye

Tumpendaye

Aliyetoa mwili wake

Akikubali mateso.

Twakupa mioyo yetu

Mwokozi uliyetufia,

Twapenda kuwa wako tu.

Bwana tukubali!

Ututengeneze sisi wako.

Nuru yako itung’aze

Tusipotee gizani,


Sisi hatukukuita,

Ila umetuita wewe,

Huruma yako ni kubwa.

Nguvu zetu hazitoshi,

Kukufanyia kazi njema

Usipotutia nguvu.

Shida yetu sisi

Ndio ulegevu, uondoe;

Nia zetu zigeuzwe

Tufanye kazi kwa bidii.


Yesu, wewe umesema:

‘’Watenda kazi ni wachache

Kweny mavuno ya Bwana’’

Twaomba: Tutume nasi,

Tualike wageni wengi,

Nyumba ya Bwana ijae.

Heri watu wale

Uliochagua kuja kwako

Kwenye raha na furaha,

Milele hata milele.


Uwahurumie watu

Walio mbali na wokovu

Wanaoshikwa nagiza.

Hawajasikia bado

Utume mwema wa wakovu

Tunaopewa na Mungu.

Jua la uzima

Liche hata kwao.

Njoo Mwokozi!

Tangulia! Twafuata,

Ukifungua milango.


Tunataka kutangaza

Habari ya upendo wako,

Ya moyo wako wa kweli

Tutawaonyesha watu

Msalaba wako siku zote,

Mpaka washindwe mioyoni,

Kwani neno lako

Lina nguvu kubwa ya

Kushinda.

Mzigo wako ni mwepesi.

Mlango wa mbinguni ni wazi.

Comments

Popular posts from this blog

72. Tumesikia Mbiu

51. Yesu Ndiye Kiongozi Wangu