53. Tumshukuru, Tumsifu
K: Tumshukuru, tumsifu
Mungu kwani ni mwema.
W: Huruma yake ipo,
Mchana na usiku.
K: Tangaza jina lake,
Mungu wetu wa kweli.
W: Huruma yake…….
K: Kajaza maajabu,
Mbinguni duniani.
W: Huruma yake……..
K: Kwa uwezo wake
Mkuu,
Ameviumba vyote.
W: Huruma yake……..
K: Aliongoza watu,
Ugenini zamani.
W: Huruma yake…..
K: Maskini katupa,
Hapa ulimwenguni.
W: Huruma yake…….
K: Anawalisha watu, hata
Wanyama pia.
W: Huruama yake…….
K: Na tumwimbie Mungu,
Kwani yeye ni mwema.
W: Huruma yake….
Comments
Post a Comment