52. Jina Lake Yesu Tamu



Jina lake Yesu tamu;

Tukilisikia

Hutupoza, tena hamu

Hutuondolea.


Roho iliyoumia

Kwalo hutibika,

Chakula, njaa pia;

Raha, tukichoka.


Jina hili ni msingi,

Ngao, ngome, mwamba,

Kwa hili Napata wingi

Kwangu ni akiba.


Yesu, Mchunga, Rafiki,

Mwalimu, kuhani,

Mwanzo, Mwisho, njia, Haki,

Uzima kifoni.


Moyo wangu hauwezi

Kukusifu kweli,

Ila sifa zangu hizi,

Bwana zikubali.

Na utakaponiita,

Kuja kwako Bwana,

Huko kwako sitaacha

Kukusifu sana.

Comments

Popular posts from this blog

72. Tumesikia Mbiu

51. Yesu Ndiye Kiongozi Wangu