48. Yesu Mponya tu Hapa
Yesu mponya tu hapa,
Moyo watulia,
Mawazo yetu yote
Uyavute kwako.
Mwanga wa neno lako,
Utuangaze wote,
Tuwe na mwangazo.
Kaa karibu na sisi,
Tunakutamani,
Mfunzi wetu ni wewe,
Sisi wanafunzi.
Nenolo lina nguvu,
Litatufanya wapya,
Laongoza vema.
Tuna furaha kubwa,
Tunakungojea.
Wewe u mwamba wetu
Tutegemeao.
Bwana tunakushika
Mpaka tunapofika
Uzimani kwako.
Comments
Post a Comment