46. Twendeni Tumshukuru



Twendeni tumshukuru

Na kumwimbia Mungu,

Aliyetupa roho

Na nguvu mpaka leo.


Twaenda na kukua

Miaka yetu yote,

Hivyo mwaka kwa mwaka

Twafikia uzee.


Twaona shida nyingi,

Uchungu na mateso

Na vita na misiba

Katika ulimwengu.


Kuhangaika kwetu

Siku zote ni bure

Asipotushikiza

Yeye atulindaye,


Na kama mama mwema

Anavyomlinda mtoto

Katika shida zote,

Asipotee njia.


Hivyo na Mungu wetu

Hulinda watu wake,

Huwakingia shida,

Huzuni na misiba.


Huruma zako ni mpya

Kila panapokucha,

Hizo zinakomesha

Uchungu wa mioyo.


Utabariki sote

Katika njia zetu,

Wakubwa kwa wadogo

Wakalishe mwangani.


U baba wa wakiwa,

U mshauri wa wajinga,

U mponya wa wagonjwa,

U msaada wa maskini.


Na mwisho twakuomba;

Utupe roho yako,

Atufundishe hapa,

Atuongoza kwako.


Wewe mwenye uzima

Utupe haya yote

Sisi wakristo wako!

Kwani twakungojea!

Comments

Popular posts from this blog

72. Tumesikia Mbiu

51. Yesu Ndiye Kiongozi Wangu