44. Mjini Mwake Daudi



Mjini mwake Daudi

Bandani mwa mifugo

Mtoto alizaliwa

Na mamaye maskini

Mariumu ni mama

Yesu mwanawe mwema.


Yesu akawa mbinguni

Akatoka enzini

Hakukaribishwa chini

Akalazwa horini

Akaja kimaskini

Kuketi duniani.


Siku za ujana wake

Akimheshimu mama

Na kumtii katika yote

Kama alivyosema.

Kila mwana na awe

Mtii kama yeye.


Amekuwa hata sasa

Kielelezo chetu

Alikuwa na unyonge

Kama unyonge wetu

Kucheka na kulia

Ni kama sisi sote.


Tutamwona waziwazi

Ndiyo ahadi yake

Sasa aketi mbinguni

Katika enzi yake

Sote na tumwandame

Kwani ni Mfalme wetu.


Tumwona Yeye tena!

Si katika kibanda,

Ila juu: nasi sote

Kwake tutakutana,

Hivyo tutasimama

Mbele yake daima.

Comments

Popular posts from this blog

72. Tumesikia Mbiu

51. Yesu Ndiye Kiongozi Wangu