40. Tushangilie Sote
K: Tushangilie sote
W: Kila mtu.
K: Mwana wa Mungu
Akaja
W: Hata kwetu
K: Tumjue Mungu Baba
W: Wa huruma.
K: Usiku wa manane
W: Shangwe kubwa.
K: Alipozaliwa Kristo
W: Awe Mfalme.
K: Pale katika mji
W: Wa Daudi.
K: Kwenye kondoo hata
Ng’ombe
W: Bethlehemu.
K: Na akaitwa kwa jina
W: La ajabu
K: Nalo Yesu Mwokozi
W: Mungu nasi
K: Hakika ni Mwokozi
W: Mwenye enzi.
K: Tupatiwe uzima
W: Wa milele
K: Na kumtumikia
Daima
W: Siku zote.
K: Maana kwake sasa
Tumemwona
W: Mungu wetu
K: Na hiyo hata
Roho
W: Mtakativu
K: Njoni kwa hiyo
Tumsifu
W: Bila mwisho
Comments
Post a Comment