37. Sote Tufurahi
K: Sote tufurahi,
W: Habari ni njema
K: Njoni nyote wahi,
W: Tupate uzima.
Sasa yametimia
Yaliyotabiriwa.
Mwokozi kazaliwa.
K: Kule Bethlehemu
W: Yesu kazaliwa
K: Mama Mariamu
W: Alivyoambiwa.
Sasa yametimia….
K: Kumbe, huyo Mwana
W: kazaliwa horini
K: Huyo Yesu Mwana
W: akawa shidani.
Sasa yametimia…
K: Mwana atiiye
W: ni Bwana shujaa,
K: Kwake tuwe wana,
W: ni Mponya dunia.
Sasa yametimia….
K: Jeshi la mbinguni
W: katoa Injili.
K: Watu walishoni,
W: kaona ni kweli.
Sasa yametimia…
K: Mungu yupo nasi
W: katika dunia.
K: Pendo kwa waasi,
W: katoa kwa nia.
Sasa yametimia…..
K: Raha na tushike,
W: tunaye Masihi
K: Haya twende kwake
W: sauti zasihi.
Sasa yametimia…..
K: Wote wenye Mwana
W: wanao uzima.
K: Yeye ndiye Bwana,
W: atoa karama.
Sasa yametimia…..
K: Nyota yatunuka
W: shinani mwa Yese
K: Bwana atukuka,
W: akatutakase.
Sasa yametimia...
K: Sasa, ndugu nyote,
W: tangaza neema.
K: Waje kwake wote
W: tupate rehema.
Sasa yametimia….
Comments
Post a Comment