36. Mwema, Mwema,Mwema
Mwema, mwema,
Mwema ni
Bwana mbinguni,
Na utengemano
Kwa watu wanaompendeza,
Kwa watu wanaompendeza.
Mwema ni Bwana mbinguni.
Mwema ni Bwana mbinguni,
Nchi itengemane,
Watu wapendezwe
Wote wakampendeze
Bwana.
Mwema,mwema,mwema
Ni Bwana mbinguni
Na utengemano
Kwa watu wanaompendeza
Kwa watu wanaompendeza!
37. Sote Tufurahi
K: Sote tufurahi,
W: Habari ni njema
K: Njoni nyote wahi,
W: Tupate uzima.
Sasa yametimia
Yaliyotabiriwa.
Mwokozi kazaliwa.
K: Kule Bethlehemu
W: Yesu kazaliwa
K: Mama Mariamu
W: Alivyoambiwa.
Sasa yametimia….
K: Kumbe, huyo Mwana
W: kazaliwa horini
K: Huyo Yesu Mwana
W: akawa shidani.
Sasa yametimia…
K: Mwana atiiye
W: ni Bwana shujaa,
K: Kwake tuwe wana,
W: ni Mponya dunia.
Sasa yametimia….
K: Jeshi la mbinguni
W: katoa Injili.
K: Watu walishoni,
W: kaona ni kweli.
Sasa yametimia…
K: Mungu yupo nasi
W: katika dunia.
K: Pendo kwa waasi,
W: katoa kwa nia.
Sasa yametimia…..
K: Raha na tushike,
W: tunaye Masihi
K: Haya twende kwake
W: sauti zasihi.
Sasa yametimia…..
K: Wote wenye Mwana
W: wanao uzima.
K: Yeye ndiye Bwana,
W: atoa karama.
Sasa yametimia…..
K: Nyota yatunuka
W: shinani mwa Yese
K: Bwana atukuka,
W: akatutakase.
Sasa yametimia...
K: Sasa, ndugu nyote,
W: tangaza neema.
K: Waje kwake wote
W: tupate rehema.
Sasa yametimia….
Comments
Post a Comment