36. Mwema, Mwema,Mwema



Mwema, mwema,

Mwema ni

Bwana mbinguni,

Na utengemano

Kwa watu wanaompendeza,

Kwa watu wanaompendeza.

Mwema ni Bwana mbinguni.

Mwema ni Bwana mbinguni,

Nchi itengemane,


Watu wapendezwe

Wote wakampendeze

Bwana.

Mwema,mwema,mwema

Ni Bwana mbinguni

Na utengemano

Kwa watu wanaompendeza

Kwa watu wanaompendeza!


37. Sote Tufurahi


K:  Sote tufurahi,

W: Habari ni njema

K:  Njoni nyote wahi,

W: Tupate uzima.

Sasa yametimia

Yaliyotabiriwa.

Mwokozi kazaliwa.


K:  Kule Bethlehemu

W: Yesu kazaliwa

K:  Mama Mariamu

W: Alivyoambiwa.

Sasa yametimia….


K:  Kumbe, huyo Mwana

W: kazaliwa horini

K:  Huyo Yesu Mwana

W: akawa shidani.

Sasa yametimia…


K: Mwana atiiye

W: ni Bwana shujaa,

K:  Kwake tuwe wana,

W: ni Mponya dunia.

Sasa yametimia….


K:  Jeshi la mbinguni

W: katoa Injili.

K:  Watu walishoni,

W:  kaona ni kweli.

Sasa yametimia…


K:  Mungu yupo nasi

W: katika dunia.

K:  Pendo kwa waasi,

W: katoa kwa nia.

Sasa yametimia…..


K:  Raha na tushike,

W: tunaye Masihi

K:  Haya twende kwake

W: sauti zasihi.

Sasa yametimia…..


K: Wote wenye Mwana

W: wanao uzima.

K: Yeye ndiye Bwana,

W: atoa karama.

Sasa yametimia…..


K:  Nyota yatunuka

W: shinani mwa Yese

K:  Bwana atukuka,

W: akatutakase.

Sasa yametimia...


K: Sasa, ndugu nyote,

W: tangaza neema.

K:  Waje kwake wote

W:  tupate rehema.

Sasa yametimia….

Comments

Popular posts from this blog

72. Tumesikia Mbiu

51. Yesu Ndiye Kiongozi Wangu