34. Wakristo Furahini
Wakristo furahini,
Furahini sana!
Mwaipigiwa leo
Mbiu yenu njema!
Malaika wanaimba
Huko juu mbinguni,
/:wanaimba vizuri
Sauti ya kushangaa!:/
Hivi wanavyoimba:
Furahini nyote!
Acheni kuogopa,
Tazama nyote
Kwani amezaliwa
Mwokozi wa pekee:
/: ni Bwana Yesu Kristo,
Mwana Mungu wetu!:/
Shangilieni nyote
Na kusikiliza.
Wapigieni nyote
Mbiu na sauti kuu.
Mungu katupa sote
Motto wa mbinguni,
/: kwa kutupenda sisi
Amekuja kwetu. :/
Comments
Post a Comment