33. Niende na Wachungaji



Niende na wachungaji

Nimtazame mponya wangu,

Kazaliwa duniani

Kwa kunipenda mimi.


Nimwimbie na malaika,

Niusifu utukufu.

Anautengemaza

Kila moyo unipende.


Nikawaze na Maria

Jambo hili la ajabu:

Acha mwili mzuri,

Achukua wa kimtu.


Nimpelekee vipaji

Na watambuzi wa nyota,

Na nimpe maji yangu,

Hata uzima nimpe.


Nakupenda, u Mwokozi,

Nikumbuke siku hii.

Uje mwangu moyoni,

Uufanye kikao.

Comments

Popular posts from this blog

72. Tumesikia Mbiu

51. Yesu Ndiye Kiongozi Wangu