24. Ulimwenguni Pote



Ulimwenguni pote

Asifiwe Mungu mkuu

Amemtuma Mwokozi,

Wakosaji wapone.


Zamani wazee wale

Wameona hamu kuu,

Waondoshwe makosa

Na kumpata Mwokozi.


Abrahamu, Yakobo

Na watu wa sayani

Walimngojea sana,

Sasa umetujia.


Karibu mponya wangu

Niondolee woga.

Ujitengenezee

Njia moyoni mwangu.


Safisha nyumba yako

Umfukuze Shetani,

Yule nyoka wa kale.

Nikutumikie wee!

Comments

Popular posts from this blog

72. Tumesikia Mbiu

51. Yesu Ndiye Kiongozi Wangu