21. Watoto Njooni Bethlehemu



Watoto njooni,

Bethlehemu,

Njooni zizini kuona makuu

Mungu aliyotutendea leo,

Watoto waone furaha

Kubwa.



Twaona kitoto kizuri

Hapa, wazee wamtazama,

Wanafurahi?

Wachungaji wote

Wanangukia,

Malaika wa mbingu

Wanamwimbia.


Pigeni magoti na

Wachungaji!

Wakubwa, wadogo

Tumnyenyekee!


Sasa popote patengenezwe,

Na watu wote watapendezwa.

Furahini!


Tuimbe na sisi  kwa

Furaha kuu

Nyimbo za kumsifu

Mwokozi Yesu!


Watoka mbinguni

Utuokoe,

Waona uchungu sababu

Yetu,

Leo wazaliwa na mwana

Kikiwa.

Halafu wateswa, unatufia.


Twapenda kukupa mioyo

Yetu,

Twataka kukutumikia vema.

Takasa mioyo ikupendeze,

Tupate kufika kwako

Mbinguni.

Comments

Popular posts from this blog

72. Tumesikia Mbiu

51. Yesu Ndiye Kiongozi Wangu