180. Bwana, u sehemu yangu
1. Bwana, u sehemu yangu, rafiki yangu wewe; katika safari yangu nitembee na wewe. Pamoja na wewe, pamoja na wewe, katika safari yangu nitembee na wewe.
2. Mali hapa sikutaka ili niheshimiwe, yanikutapo mateso sawasawa na wewe. Pamoja na wewe, pamoja na wewe, heri nikute mateso sawasawa na wewe.
3. Niongoze safarini, mbele unichukue. Mlangoni mwa mbinguni niingie na wewe.
Pamoja na wewe, pamoja na wewe, mlangoni mwa mbinguni niingie na wewe.
Comments
Post a Comment