153. Ninapenda Kwenda Zangu
1. Ninapenda kwenda zangu
nimwone Mwokozi wangu.
Moyo wangu watamani
kuambatana na Yesu
/: na kumsifu milele
2. Ninapenda kusikia
nyimbo za malaika wote.
Ningekuwa na mabawa
Ningeruka leo hivi
/: mpaka Sayuni kwake:/
3. Ninapenda kuingia
pale penye utukufu,
penye nyumba za dhahabu
nimwone Mwokozi
wangu
/: na furaha za mbingu :/
4. Ninapenda kuuona
uzuri wa Paradiso.
Nikifika nitapata
tunda lake tamu sana,
/:Yesu, nipeleke juu!:/
Comments
Post a Comment