15. Tawi Limechipuka



Tawi limechipuka

Shinani mwa Yese,

Kama tulivyopashwa

Habari na wazee.

Likatoa ua

Wakati wa usiku

Lilipochanua.


Isaya alitaja ua hilo zuri.

Ni Yesu, mponya wetu,

Maria alimzaa

Usiku mtulivu.

Uwezo wake Mungu

Umefanya hivi.


Na ua hili dogo

Lanukia vyema;

Lang’aa kama jua

Giza lakufukuzwa.

Ni Mwana wa Mungu,

Hata mwana Adamu;

Mwokozi wa watu.


Siku ya kufa kwetu

Yesu tuongoze,

Tuiache dunia,

Twende furahani

Mbinguni kwa Mungu

Pale tuta kusifu

Pasipo kukoma.

Comments

Popular posts from this blog

72. Tumesikia Mbiu

51. Yesu Ndiye Kiongozi Wangu