148. Mungu Baba, Mungu Mwana
1. W: Mungu Baba, Mungu Mwana, Mungu Roho, twakusifu twakushangilia sote, umejifunua kwetu kwa upendo, kwamba wanadamu wakujue wote. K: Mungu wetu W: Anapenda tuwe wake K: Dhambi zetu W: Tuache, tumfuate.
2. W: Mungu Baba wewe uliumba vyote, mbingu, dunia na vilivyomo vyote, watu, ndege na wanyama uliumba, jua, mwezi na nyota vyakutukuza. K: Mungu wetu
3. W: Mungu Mwana, wewe ulikuja kwetu ukaishi kama mwanadamu kweli, ukateswa na kubeba dhambi zetu, kwamba sisi tupate wokovu kweli. K: Mungu wetu
4. W: Mungu Roho, uliye kiungo chetu wakusanya na kuita watu wote, tufundishe kumjua Bwana wetu, na utukufu wake hata milele. K: Mungu wetu.
Comments
Post a Comment