Tumesikia mbiu: Yesu, loo! Aponya; Itangazeni kote, Yesu loo! Aponya. Tiini amri hiyo: Nchini na baharini, Enezeni mbiu hii: Yesu loo! Aponya. Imbeni na vitani: Yesu loo! Aponya; Kwa nguvu ya Mkombozi, Yesu loo! aponya. Imbeni wenye shida, Unapo umwa moyo, Na kaburini imba: Yesu, loo! Aponya. Mawimbini ienee: Yesu, loo! Aponya Wenye dhambi jueni: Yesu, loo! Aponya Visiwa na viimbe, Vilindi itikeni, Nchi shangilieni: Yesu, loo! Aponya. Upepo utangaze: Yesu, loo! Aponya; Mataifa yashangaa; Yesu loo! Aponya. Milimani, bondeni, Sauti isikike Y wimbo wa washindi: Yesu loo! Aponya.
Yesu ndiye kiongozi Wangu, Kumfuata yeye ni furaha, Ajuaye kuongoza vema, Anilinda, nisione shida, Analeta raha moyoni. Bwana yesu Akiniogoza, Nitapita pori na misitu, Nitavuka mito na bahari Kwa furaha, Kwani nina njia Yakufika mjini kwa Mungu. Nikilala Yesu anilinda, Anitunza yeye siku zote. Hata nikifika njia panda, Nikiona shaka, aonyesha Njia ya kufika kwake. Siku zote namfuata yeye, Sitaona kiu wala njaa; Anitunza kwa rehema Nyingi; Nitaweka mikononi mwake Moyo wangu, auokoe.
Mwenyezi, Mwenyezi, Mwenyezi, jina lako litukuzwe sana. Amin, amin. Hata ulimwengu wetu utekelezwe kwa moto. Nazo nyumba zetu, ziimbe utakatifu wake, haleluya, haleluya.
Comments
Post a Comment