119. Bwana Amefufuka, Haleluya
1. Bwana amefufuka, haleluya. Tuimbe na amlaika, haleluya. Sifa zetu na shangwe, haleluya. Na zao zisitengwe. Haleluya.
2. Ukombozi timamu, haleluya. Umetimu kwa damu, haleluya. Mshindi asifiwe, haleluya. Yu hai kwa milele, haleluya.
3. Jiwe, lindo, muhuri, haleluya vi wapi? Na kaburi? Haleluya. Kifo hakimuwezi, haleluya. Ametoka kuzimu, haleluya.
4. Yu hai mtukufu, haleluya. Cha kifo hatuofu! Haleluya. Alitufia sisi, haleluya. Tuwe huru na sisi, haleluya.
5. Kichwa chatangulia, haleluya. Tupate, nasi pia! Haleluya. Kw akuwa tuna fungu, haleluya. Mti, kaburi mbingu, haleluya.
6. Ndiwe mwokozi wetu, haleluya. Sifa ni yako Yesu, haleluya. Utukuzwe pekee, haleluya. Ni wewe ufufuo, haleluya.
Comments
Post a Comment