114. Amefufuka Katika Wafu
1. K: Amefufuka katika wafu, akiwa na utukufu.
Kristo pekee, ndiye mwenye nguvu.
W: Yeye limbuko la waliolala,
tena ni mwisho wa nguvu ya mauti kwetu.
2. K: Hii ni habari iliyo kweli, iletayo udhahiri.
Yapasa wote, tuache mashaka.
W: Yesu pekee ndiwe ustahiliye kushika mamlaka yote.
3. K: Kristo u Bwana mwenye uweza.
Shetani umemshinda, kazi yote umeimaliza.
W: Uhimidiwe, ewe Bwana pekee, utupokee tunapokuja kwako, Bwana.
4. K: tuutangaze ushindi wake,
mataifa waje kwake,
wafahamu utukufu wake.
W: Asante, Bwana, kwa ushindi wako kwa watu wako. Shetani hana nguvu tena.
Comments
Post a Comment