112. Leo Siku ya Furaha



Leo siku ya furaha,

kila mtu ashangilie,

Kristo afufuka, ateka

adui wote! Haleluya!


Nyoka wa kale na kifo,

kuzimu hata ubaya vimeshindwa

na mshindaji Yesu Kristo

Mfalme wetu! Haleluya!


Mateka yote ya kifo

yamekamatwa na Yesu,

na ufu umenyang’anywa

naye aliyefufuka! Haleluya!


Adui hawatushiki tunakwenda

uzimani, tunapokunywa naye

kinywaji kipya milele! Haleluya!


Jua na mwezi na nchi, viumbe

vyote vya Mungu vinafurahiwa

leo; Mfalme wa uongo ashindwa!

Haleluya!


Kwa hivi tushangilie,

tumwimbie Yesu Kristo,

yeye ametuokoa, afufuka

kaburini! Haleluya!

Comments

Popular posts from this blog

72. Tumesikia Mbiu

51. Yesu Ndiye Kiongozi Wangu