110. Haleluya, Haleluya
Haleluya, Haleluya,
sauti na mioyo juu,
tumwimbie Mungu nyimbo
tumsifu na furaha, aliyemwaga
damuye kwa ulimwengu wote,
mefufuka kifoni sas Yesu Mwokozi.
Minyororo yake kifo imekatika
pia, na katika wafu wote
yee mzaliwa wa kwanza Yesu
ameshinda sasa, nasi twashinda
naye. Ametupatia nasi
uzima wa milele.
Kristo afufuka kwanza nao
wengi baadaye. Atakapokuja tena,
watatokea naye, mavuno yatakuwako
mwisho wa ulimwengu,
watafika furahani wote watakatifu.
Mwokozi amefufuka, nasi tutafufuka,
tunyeshee kama mvua neema yako ee Bwana.
Tutafute yaliyo juu, siyo ya ulimwengu,
na uzima tutapewa naye Kristo kwa Mungu.
Tumsifu, tumsifu Mungu wetu, apaswa.
Tumsifuni na Mwokozi, aliyeshinda vita.
Tumsifu naye Roho, kisima cha mapenzi.
Tumsifu Mungu wetu, ni Utatu wa enzi.
Comments
Post a Comment