108. Tumfurahie Daima
Tumfurahie daima, Yesu
aliyefufuka Haleluya! Haleluya!
Giza haliwezi kukaa, jua limelifukuza.
Haleluya!Haleluya!
Haleluya!Haleluya!Haleluya
Nao moyo wa Maria, unashangilia
sana, Haleluya! Haleluya!
Nayo mioyo yetu sisi,
inapiga shangwe nyingi! Haleluya!.
Jeraha zake za kufa, zatupatia uzima,
Haleluya!Haleluya! Na sasa anatawala
katika enzi ya Baba. Haleluya!
Mwokozi hakuogopa, kuvuka maji ya kufa,
Haleluya! Haleluya! Atupa nasi
moyo mkuu, Tuongoze tufike juu!
Haleluya!
Comments
Post a Comment