102. Haleluya Tumwimbie



Haleluya! Tumwimbie tumsifu

sana Bwana wetu, tumshangilie

kwa shangwe. Akafungwa na adui

alipokufa msalabani,

lakini sasa yu hai.

Habari njema hii: Mesiya anakaa

mzima kweli. Haleluya!

Tumsifu! Tumsifu! Mungu wetu.


Haleluya! Tumwimbie,

tumsifu sana Bwana wetu,

tumshangilie kwa shangwe.

Watu wana shida sana,

taabu nyingi na huzuni mpaka

watakapokufa. Furaha yetu hii;

Bwana ametoka kaburini.

Haleluya! Tumsifu!

Tumsifu Mungu wetu!


Haleluya! Tumwimbie,

tumsifu sana Bwana wetu,

tumshangilie kwa shangwe.

Atatufufua sisi,

tutafika rahani kwake,

tuishi pamoja naye.

Tumwamini yeye Mwokozi wetu mkuu,

mwenye nguvu. Haleluya!

Tumsifu! Tumsifu Mungu wetu!

Comments

Popular posts from this blog

72. Tumesikia Mbiu

51. Yesu Ndiye Kiongozi Wangu