101. Moyo Wangu Amka Hima



Moyo wangu amka hima,

jua limetokea. Ondoka usingizini,

mpokee Mponya wako,

atokaye kaburini,

kashinda nguvu za kifo,

watu wafurahishwe.


Fufuka pamoja naye,

uyaache mabaya! Maliza mwenendo

wako ukimgojea Yesu, aliyekwenda

mbinguni.

Kwa hiyo nawe ufanye yampendezayo yeye.


Ukiwa na wasiwasi Yesu anauweza;

Ukipatwa na huzuni, yeye furaha yako.

Umtwike Bwana mizigo.

Usisumbuke: yu hapa, kwani amefufuka.


Usimwogope Shetani,

kifo hata kuzimu.

Shida za kufa nyepesi mwokozi

Yesu ni mzima. Shujaa wetu haondoki,

awagombea wanyonge wanaomtumaini.

Comments

Popular posts from this blog

72. Tumesikia Mbiu

51. Yesu Ndiye Kiongozi Wangu