100. Mungu Tusaidie
Asili ya Wimbo: Haijulikani
Mungu tusaidie,
sisi tunaangamia.
Nchi imeharibiwa na
mwovu wake shetani.
Kweli kweli ndiye
Yesu aliyewambwa mtini
penye mlima wa Golgotha
aokoe wenye dhambi.
Kaonyesha huruma,
wayuda wamsumbua.
Wakampiga makofi,
Pilato aliamua.
Kweli kweli ndiye Yesu
Yesu mwenye upendo
alikubali kuuawa, damu ilimwagika
ili sisi tuokoke.
Kweli kweli ndiye Yesu.
Pale msalabani, Bwana Yesu
aliteswa mzigo wa dhambi zetu
ulimwangukia yeye.
Kweli kweli ndiye Yesu
Sote na tukumbuke,
kifo cha Mwokozi wetu.
Alisema ya kwamba jililieni wenyewe.
Kweli kweli ndiye Yesu
Habari zilisemwa.
Mahali hapa hayupo, ona alipokuwa,
jiwe limeondolewa.
Kweli kweli ndiye Yesu
Ni ajabu kabisa wingu kuja kumpokea,
habari ilisema Yesu atarudi tena.
Kweli kweli ndiye Yesu
Comments
Post a Comment