10. Bwana Anakuja



Bwana anakuja

Twendeni kumlaki

Bwana wangu wa majeshi.

Iwasheni mioyo

Tukampokee

Huyo mwenye utukufu.

Karibu Bwana, njoo

Karibu Bwana, njoo

Shinda pamoja nasi.


Wewe ndiwe mfalme,

Mfale wa mbinguni

Utulishe wenye njaa.

Wewe ndiwe mwanga,

Sisi tu vipofu

Tufanye tuone tena


Wewe ndiwe njia,

Tuta kufuata

Turudi kwa baba yetu.

Wewe ndiwe kweli,

Utuangazie

Tusije tukapotea.


Hosanna, Hosana,

Huyo mbarikiwa

Anakuja kwetu sisi.

Aja kutulisha na kutugawia

Matunda ya ukombozi.

Comments

Popular posts from this blog

72. Tumesikia Mbiu

51. Yesu Ndiye Kiongozi Wangu